JIFUNZE KUCHEZA NA RANGI YA VIPODOZI KATIKA KUKAMILISHA UREMBO WAKO


UREMBO NI MAISHA, YAPO MAMBO MBALIMBALI YANAYOWEZA KUKUONGEZEA MVUTO KATIKA MUONEKANO WAKO



Moja ya mambo hayo ni ujuzi na uelewa wa kutumia rangi katika kujipodoa kwani ni wanawake wachache wenye ujuzi huu.

Katika makala hii, nitakuelezea namna ya kuchanganya na kutofautisha rangi za vipodozi, lengo likiwa ni kuboresha muonekano wako.

Uchanganyaji wa rangi za vipodozi ni muhimu sana kwani katika kujipodoa, rangi zote za vipodozi unavyopaka zinatakiwa zioane ili kuleta muonekano ulio sawa na wa kueleweka.

FAITH MSUYA, katika moja ya events.

Kwanza kabisa unatakiwa uwe makini katika kuoanisha rangi za vipodozi pamoja na rangi ya ngozi yako, hivyo katika hili unatakiwa kuwa na ujuzi maalumu ili usije ukafanya makosa na kuharibu muonekano wako.

Pia inabidi ufahamu hatua za upakaji vipodozi ili usije ukafanya vipodozi vingine visionekane katika uso wako.
Namna ya kuoanisha na kutofautisha rangi.

Siku zote vipodozi vyako lazima viendane na mavazi yako ili kuleta maana zaidi kwa mfano, mara nyingi rangi ya mdomo ‘lipstick’ huendana na vazi lako wakati shedo ‘eye shadow’ zinatofautiana.

Kwa nguo za pinki

Katika mavazi haya, unatakiwa kupaka rangi ya mdomo yenye rangi ya pinki ambayo itaendana sawasawa na mavazi yako huku ukichanganya na shedo ‘eyeshadow’, inaweza kuwa ya rangi ya bluu ili kuitofautisha na mavazi yako, hapo utakuwa sawa katika kanuni za urembo.

Vazi la kijani

katika vazi hili unatakiwa kupaka rangi ya mdomo yenye rangi ya kahawia huku ukichanganya na shedo ya rangi ya kijani au kahawia iliyoingiliana na pinki au rangi ya machungwa. 

Kwa vazi la njano au kahawia 
Katika vazi hili unatakiwa kupaka ‘lipstick’ ya rangi ya kahawia iliyokolea, kwa upande wa shedo waweza kupaka ya rangi ya dhahabu.

Kwa vazi la bluu 
Katika vazi hili unatakiwa kupaka ‘lipstick’ yenye rangi ya pinki huku ukipaka shedo ya rangi ya bluu kwa mtindo huu utakuwa mwenye kuvutia siku zote.

Rafiki, hakuna (uchawi) linapokuja suala la kupendeza, ni ubunifu na akili yako zinapaswa kutenda kazi vyema ili kuweza kukuweka uwe mwenye muonekano wa kuvutia mara zote.
Ulikuwa nami Faith Msuya, tukutane wakati ujao!!!
Kwa maoni,
0766 641 185
Facebook @ Faith Msuya
Instagram @ FaithMsuya
Email | iamfaithmsuya@gmail.com

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

JINSI YA KUONGEZA KUJIAMINI KATIKA MAISHA YAKO

TAFSIRI YA UREMBO